Saturday, November 29, 2014

MAAZIMIO YA BUNGE JUU YA SAKATA LA ESCROW

Baada ya Sakata la ESCROW kuchukua muda mrefu katika mijadala wa vikao vya Bunge hatua iliyopelekea Bunge kuweka historia ya kuendelea na kikao chake jana tarehe 28/11/2014 hadi saa tano Usiku. Aidha katika kikao hicho hakikumalizika kwa hali nzuri kutoka na na Baadhi ya wabunge wa CCM kuonekana waziwazi wakiwatete Watuhumiwa wa wizi wa mabilioni ya fedha za ESCROW.

Katika hatua nyingine leo tarehe 29/11/2014 iliundwa kamati maalum iliyojumuisha PAC, CCM na UKAWA ambapo kwa niaba ya Bunge walifikia maazimio yafuatayo ambayo baadaye saa 7:00 Jion yalisomwa Bungeni na kuridhiwa na wabunge walio wengi.

1.BUNGE LINAAZIMIA KUWA WOTE WALIOHUSIKA WAWAJIBIKE NAKUWAJIBISHWA KWA MUJIBU WASHERIA

2.SERIKALI IANGALIE UWEZEKANO WA KUTAIFISHA NA KUFANYA MITAMBO YA IPTL SASA IMILIKIWE NA SERIKALI

3.SERIKALI IPITIE UPYA MIKATABA YOTE NA KUANGALIA KAMA INAMASLAHI NA TAIFA,NA IBORESHWE.

4.SERIKALI ILETE MUSWADA WAKUREKEBISHA SHERIA YA TAKUKURU ILI KUUNDA CHOMBO KINGINE KITAKACHOKUWA NA NGUVU ZAIDI YA KUPAMBANA NA RUSHWA KUBWA KUBWA

5.MAJAJI WALIOTAJWA KUHISIKA INAPENDEKEZWA KUWA MH RAIS AUNDE TUME YA KIJAJI KUWACHUNGUZA JAJI ALOIS NA JAJI LUHANGISA NA KISHA WACHUKULIWE ATUA

6.BANK YA STANBIC BANK TZ LTD NA BANK NYINGINE ZOTE ZILIZOHUSIKA KATIKA KUTAKATISHA PESA HARAMU ZA KAMPUNI ZA (PAP NA VIP LTD) NI JINAI NA BANK HIZO ZOTE ZITANGAZWE NA MAMLAKA HUSIKA KUWA NI BANK ZENYE SHAKA YA UTAKATISHAJI NA UPOKEAJI WA PESA HARAMU

7.BUNGE LINASHAURI NA KUAZIMIA WAZIRI WA MADINI, WAZIRI WA ARDHI,MWANASHERIA MKUU,KATIBU MKUU WA WIZARA YA NISHATI NA MADINI,WAWAJIBISHWE NA MAMLAKA YA UTEUZI ITENGUE UTEUZI WAO.

8.WENYEVITI WA KAMATI ZA BUNGE AKIWAMO MH NGELEJA WANAOTAJWA KUHUSIKA WAVULIWE UENYEKITI NA NAFASI ZAO KAMATI HUSIKA ZICHUKUE HATUA HARAKA KUWAVUA NAFASI ZAO

Nawapongeza wabunge wote kwa kuondoa tofauti zao na kujali maslai ya taifa!!!!!

Sunday, September 14, 2014


"POLITICAL TOLERANCE" Siasa ni kuvumiliana na siyo uadui
Ni Kauli ya Makamu M/Kiti Taifa
Ndg Phillip Mangula katika Mkutano Mkuu wa CDM
akimwakilisha Rais ni vyema kauli hii iwe funzo kwa wanaCCM wote
na Wanzania kwa ujumla wake
hakika ni maneno ya busara na yakuonesha ukomavu
wa kisiasa Hongera sana Mzee Mangula,

Hongera sana CCM kwa kuwa na viongozi Shupavu

Friday, September 5, 2014

TOP SIGNS THAT HE'S JUST USING YOU.


Relationship advice is something you need to pay attention to if you suspect that your man is taking advantage of you. Is it true? Find out now!
Being used can be devastating to the ego and your self-esteem. If you’re in a relationship –whether budding or established and you thin that he might be taking advantage of you, you’re probably right. There are a lot of reasons that men use women. S3x is the one that most women think of, but there are others. Men cherish their self-image and having a great looking girl by their side is one of the biggest statements he can make while in public. A beautiful woman is a sign of success and power. This is a coveted feature of any man’s life, but he may only have superficial interest in you.

1. He Doesn’t Make You Feel Special
A guy that really cares about you is going to show that you’re the only girl on his mind. If you’re dating a fella that buys you generic gifts on your birthday or blows you off to spend time with his friends, he probably wants you as a backup plan. Get rid of him and get with one that will make you feel like the only girl he’s thinking about.

2. He Doesn’t Really Care Much About You
Does he ask how your day was when you walk through the door? If he does, can you tell that he’s actually interested in what you did for the last 12 hours of your life? If you sense disinterest in your work, your family or your passions, he’s probably taking advantage of you. A guy that takes a genuine interest in all of these aspects is going to respect you and really care about what is going on.

3. He Doesn’t Text Or Call You Back
If you send a text to your guy, what is his typical response time? Does he apologize if he doesn’t respond in a timely manner? If he takes a day or two to get back to you, he’s probably taking advantage of you. Men that are interested won’t leave you hanging.

4. He Has never Introduced You To His Family
If you have only been dating for a couple of weeks, you can let this one slide. But if you have been together for a couple of months and you still haven’t met his parents, there is something else going on. A man wants to have the approval of his parents. Dump him if he refuses to introduce you to his parents.

5. He Doesn’t Want To Meet Your Family
If he avoids meeting your family, this is another red flag. Meeting your family is a big deal. Looking your father in the eye while he inquires about his intentions with you is a staple of every relationship. If your guy refused to meet your family, it’s time to move on.

6. He Doesn’t Respect you
A man should always treat a lady as a lady. If he is disrespectful to you, he just wants you until you hit the breaking point. No man should ever treat a woman as anything other than an equal. Remember this the next time he makes a disrespectful remark.

Wednesday, August 27, 2014

MAMBO MUHIMU AMBAYO HAUJAWAHI KUFUNDISHWA SHULENI

Kwa miaka zaidi ya 15 ambayo umekaa kwenye mfumo wa elimu umejifunza vitu vingi sana. Kwanza ulijifunza jinsi ya kusoma na kuandika, baadae ukajifunza vitu muhimu kwenye historia, jografia, sayansi na hata mahesabu. Mwisho kabisa ukapata elimu ya utaalamu na hatimaye ukamaliza masomo yako kwenye utaalamu au ujuzi uliochagua kusoma.
Pamoja namambo hayo mengi na mazuri uliyojifunza kwa miaka hiyo mingi kuna mambo mengi sana ambayo ni muhimu kwenye maisha hukupata nafasi ya kujifunza au kufundishwa. Kutokujua mambo hayo muhimu kuhusu maisha ndio kumekuwa chanzo kikubwa cha wahitimu wengi kuona maisha ni magumu sana wanapofika mtaani.

Leo tutajadili mambo muhimu ambayo hukufundishwa shuleni ila ni ya muhimu sana kwenye maisha yako.
Mambo haya kumi muhimu ni;

1. Wewe ni wa pekee.
Katika watu zaidi ya bilioni saba wanaoishi kwenye dunia hii hakuna hata mmoja ambaye anafanana na wewe kwa kila kitu. Wewe ni wa pekee, una uwezo mkubwa sana na una vipaji na ubunifu wa kipekee. Ukishajua hili itakuwa rahisi kwako kufanikiwa kwani hutoweza kujilinganisha na mtu mwingine.
Shule imefanya kazi nzuri sana ya kukulazimisha kujilinganisha na wengine kwenye kila jambo unalofanya. Hii ni kwa sababu shuleni ulikuwa unafanya mtihani mmoja na wanafunzi wengine wote hivyo kupimwa kwa kulinganishwa.
Acha sasa kujilinganisha na wengine na tambua wewe ni wa pekee na hakuna anayeweza kufanta unayoweza kufanya wewe.

2. Unaweza kufanya chochote unachotaka.
Kwa kuwa wewe ni wa pekee, pia una uwezo mkubwa sana wa kuweza kufanya MAMBO MAKUBWA SANA. Kamwe usijishushe na kujiona wa chini, unaweza kufanya jambo lolote unalotaka kulifanya kwenye maisha yako. Unaweza kuyafanya maisha yako kuwa bora kuanzia sasa unapomaliza kusoma hapa. Kitu muhimu ni wewe kujua ni kitu gani unataka kwenye maisha yako na kukitafuta kwa juhudi na maarifa.

3. Hakuna jibu moja sahihi.
Mitihani uliyokuwa unafanya shuleni ilikulenga kuchagua jubu moja sahihi na kuacha mengine ambayo sio sahihi. Kwa bahati mbaya sana maisha hayako hivyo. Hakuna jibu moja sahihi au ambalo sio sahihi, yote ni majibu na yana usahihi na makosa kadiri maisha yanavyozidi kwenda.
Usidanganyike kwamba kuna kitu kimoja ukifata ndio utafanikiwa kwenye maisha, njia ya mafanikio ina vikwazo na changamoto nyingi. Usirudishwe nyuma na changamoto hizi kwa sababu ya mambo uliyofundishwa shuleni kwamba jibu sahihi ni moja tu.

4. Maana ya mafanikio.
Kila mtu kwenye maisha anataka kupata mafanikio makubwa, ila ni wachache sana ambao wanajua maana halisi ya mafanikio. Shuleni ulifundishwa kwamba kufanikiwa na kupita kiwango fulani cha maksi au hata kuwapita wengine darasani kwa ufaulu wa maksi.
Kwa bahati mbaya sana kwenye maisha mafanikio hayapimwi hivyo. Ukiangalia mafanikio kwa kutaka kuwashinda wengine au kuwa sawa na wengine utaishi maisha yako yote kukimbiza upepo. Maana ukijitahidi ukanunua gari kuna mtu utamkuta ana magari mengi zaidi yako, ukasema mafanikio ni kujenga nyumba kwa sababu kila mtu ana nyumba utakutana na mtu mwenye nyumba kubwa, nzuri na nyingi kuliko ya kwako. Kwa akili hii utaumia kichwa na kuona maisha yako hayana maana.
Badala ya kuendeshwa na mafanikio ya wengine kaa chini na uandike maana yako mwenyewe ya mafanikio kisha ishi kuitimiza maana hiyo.

5. Hakuna mtu yeyote au kitu chochote kinaweza kukupa furaha.
Hili ni jambo muhimu sana ambalo hukupata nafasi ya kufundishwa. Furaha inatoka ndani yako mwenyewe, hupewi na mtu au kitu unachomiliki.
Kama unafikiri mwenzi wako ndio atakupa furaha basi kuna siku utaumizwa sana, kama unafikiri fedha nyingi ndio zitakupa furaha uko kwenye tatizo kubwa. Furaha ipo ndani yako na utaipata kutokana na maisha unayoishi na mambo unayoyafanya kwako na kwa watu wengine.

6. Kufaulu darasani hakumaanishi kufaulu kwenye maisha.
Mazingira ya darasani yanatabirika, kaa darasani, soma kwa bidii, jiandae na mtihani na utafaulu. Mazingira ya kwenye maisha hayatabiriki hata chembe, unaweza kufanya kazi kwa juhudi na maarifa na bado yakatokea mambo yakakurudisha nyuma. Mitihani ya shuleni unajua ni lini inakuja hivyo unaweza kujiandaa muda huo ila mitihani ya kwenye maisha haina ratiba na hivyo inakukuta hujajiandaa. Ndio maana kufaulu darasani hakumaanishi ndio utafaulu kwenye maisha, kuna mambo mengi sana unatakiwa kujifunza.

7. Kukosea/kufeli ndio kujifunza.
Shuleni kufeli ni kwamba hujui au hujajiandaa vizuri na hivyo kukufanya uonekane wewe ni mwanafunzi dhaifu. Ila kwenye maisha kukosea au kufeli ndio njia sahihi ya kujifunza. Hujajifunza jambo lolote kweye maisha kama hujafeli au kuhsindwa kwenye jambo hilo. Badala ya kuogopa kufeli kwa sababu utaonekana ni dhaifu, hebu anza kuchukua kufeli kama sehemu ya kujifunza kwenye maisha yako.

8. Kuweka malengo.
Hiki ni kitu kimoja muhimu sana ambacho hukupata nafasi ya kufundishwa na kusisitiziwa vizuri wakati upo shuleni. Ni vigumu sana kuweza kufikia mafanikio makubwa unayotegemea kwenye maisha yako kama hutaweka malengo makubwa na mipango ya kufikia malengo yako. Kwa kushindwa kufanya hivi unawapa nafasi watu wengine wakutumie wewe kufikia malengo yao.

9. Matumizi ya fedha binafsi.
Fedha ni muhimu sana kwenye maisha yetu na huenda sababu kubwa iliyokufanya ukae shuleni miaka yote hiyo ni kupata fedha baadae. Pamoja na umuhimu huu wa fedha hukuwahi kupata nafasi ya kufundishwa matumizi na mipango binafsi ya fedha unazozipata. Hii inakusababishia kuwa na matumizi mabaya ya fedha na kuona maisha magumu kila siku.
Ni muhimu sana kuwa na matumizi mazuri ya fedha zako kwani hiki ndio kitakuwezesha kufikia mafanikio makubwa unayotazamia.

10. Haijalishi unajua nini bali unamjua nani.
Umeaminisha shuleni kwamba kama ukisoma kwa juhudi na maarifa, ukajua vitu vingi sana basi unaweza kufikia mafanikioa makubwa sana. Kujua vitu vingi sana hakuwezi kukusaidia kama huwajui watu muhimu. Hivyo kwa kuwa umeshajua vitu vingi sasa wekeza nguvu sako kuwajua watu sahihi ili kuweza kufikia malengo yako. Mafanikio yako yatatokana na watu muhimu ulionao kwenye mtandao wako. Hivyo jua watu wengi sana na muhimu zaidi jua wale ambao watakusaidia kufanikiwa kwenye taaluma au shughuli unazofanya.
Maisha halisi ni tofauti sana na mambo ambayo umekuwa ukifundishwa darasani kwa miaka mingi. Ni wakati wako sasa wa kuweza kujifunza vitu muhimu ambavyo hukufundishwa darasani.

Tuesday, August 26, 2014

MATENDO YA MSIGWA YADHIBITISHA AKILI NDOGO INAWEZA KUITAWALA AKILI KUBWA

CHADEMA WAANZISHA MGOGORO NA BODABODA IRINGA MJINI

Ni siku mbili tu zimepita toka tarehe 23/08/2014 mh Mwigulu Nchemba Naibu Katibu mkuu CCM Bara na Naibu Waziri wa Fedha alipomuapishwa komredi Salim Abri (ASAS) kuwa Kamanda wa UVCCM mkoa wa Iringa na baadae kuhutubia mkutano mkubwa wa kihistoria wa hadhara katika viwanja vya Mwembetogwa Iringa mjini.

Sherehe hizo zilishirikisha wanaCCM wengi sana wa ndani ya mkoa wa Iringa na nje,Wananchi wengi sana kutoka takribani kila kata ya Manispaa ya Iringa.Pia vijana waendesha Bodaboda kutoka vijiwe mbalimbali nao walishiriki kikamilifu kuanzia mapokezi ya Mh Mwigulu Nchemba,kumsindikiza mitaani katika ufunguzi wa mashina ya Wakereketwa na baadae kumsindikiza kwa furaha kubwa na mbwembwe nyingi hadi eneo lililofanyika mkutano.

Vijana hawa wa Bodaboda wamekuwa wakikabiliwa na matatizo na chamgoto nyingi kwenye kazi zao za kila siku na kila wanapomfuata mbunge wao waliemchagua Mch Peter Msigwa amekuwa akiwapa majibu ya dharau,kejeli na kebehi kuwa hana nafasi,ana majukumu mengi ya chama chake au hana fedha na mara nyingi huwaambia kuwa jukumu la kuwasaidia sio la kwake,hiyo ni kazi ya CCM iliyo madarakani.

CCM iliamua kubeba jukumu la kufanya kazi alizokataa mbunge huyo la kuhangaika kutatua matatizo na changamoto zinazowakabili vijana hao wa Bodaboda,ikiwa ni kwanza kuwasaidia kuunda umoja wao,kufanya uchaguzi wa kidemokrasia ili kupata viongozi wao,kufanya mazungumzo na viongozi wa Sumatra,Polisi na Halmashauri ya Manispaa kuweka mpango mzuri wa kufanya kazi zao bila kubughudhiwa na vyombo hivyo kama awali ambapo walikuwa wanafanya kazi katika mazingira magumu sana ya kukimbizana na maafisa hawa.

Pia CCM inapambana kuwatafutia mikopo na wafadhili wa kuwasaidia mitaji,akiwemo Kamanda wa UVCCM mkoa Salim Abri(ASAS) ambae amekuwa msaada mkubwa sana kwao katika shida zao mbalimbali.

Kwa kazi nzuri inayofanywa na viongozi wa CCM kuwajali na kupambana katika kushughulikia matatizo yao,vijana hawa kwa hiari yao waliamua kuwa karibu na CCM na kusaidia kufanikisha kazi mbalimbali za CCM,kama walivyofanya tarehe 23/08/2014 katika kuapishwa kwa Kamanda na katika mkutano wa mh Mwigulu Nchemba.

Kitendo cha vijana hawa kushiriki kikamilifu katika mkutano wa CCM wa mh Mwigulu Nchemba wa juzi tarehe 23/08/2014 kilionekana wazi kumkera sana mbunge Mch Peter Msigwa kwa kuona kuwa vijana wameamua kumsaliti na amehisi kuwa anazidi kupoteza kundi kubwa na muhimu la vijana ambalo awali lilikuwa likimuunga sana mkono likiamini labda angewaletea miujiza katika maendeleo na kumbe wakaishia kashfa na kutelekezwa.

Leo tarehe 25/08/2014 Bw.Msigwa akaitisha mkutano wa vijana hao wa Bodaboda katika ukumbi wa Walfare,akiwa na malengo yafuatayo:-

-Kwanza kuwajenga chuki dhidi ya CCM kwa kuwachonganisha kwa fitina kuwa eti CCM imemnunua mwenyekiti wao na imemjengea nyumba hivyo wamkatae.
-Aliwaambia eti uchaguzi waliofanya mwanzo ni batili kwa sababu mwenyekiti waliemchagua anaonekana anaisikiliza sana CCM.
-Alitoa ahadi ya shilingi Milioni tatu na kuwa atawaletea pikipiki kumi ifikapo mwezi Februari 2015 ili wafanyie kazi.
-Alitoa maagizo hapo mkutanoni kuwa mwenyekiti na viongozi wenzake wanaotuhumiwa kuitii CCM washambuliwe kwa kipigo mara moja ili iwe fundisho kwa wengine kuiunga mkono CCM.

Baada ya maelekezo hayo ya mbunge kutolewa ndipo mabaunsa wa Chadema walipoanza kufunga milango ya ukumbi ili kipigo kianze.Wale viongozi walifanikiwa kutoka nje wakikimbia na nyuma wakiandamwa na wafuasi wa Mch Msigwa na mabaunsa.

Pale nje ya ukumbi walikuwepo vijana wengine wengi wa Bodaboda ambao walizuiwa na mabaunsa kuingia ukumbini kwa madai kuwa ni vibaraka wa CCM.Vijana hawa walipoona viongozi wao wanakimbizwa na kushambuliwa,nao waliamua kuingilia kati kuwatetea.

Vurugu zilikuwa kubwa na ziliendelea kwa muda kidogo hadi Polisi walipofika eneo la tukio na kujaribu kutuliza bila mafanikio hadi walipoamua kupiga risasi kadhaa angani ndio vurugu zikatulia.

Polisi walipouliza nini kimetokea?walipewa maelezo na Bw. Msigwa kuwa huyo kijana ametumwa na CCM kuja kufanya fujo ili avuruge mkutano wao.Polisi walimchukua mwenyekiti huyo wa Bodaboda kwa kwenda nae kwa madai kuwa anaenda kuandika maelezo kituoni na baadae ataachiliwa huru.

Bw. Msigwa aliwaagiza vijana hao wakutane baada ya wiki mbili na kuwaondoa madarakani hao viongozi wanaoonekana kuiunga mkono CCM na yeye atasimamia ili wachaguliwe viongozi wengine ambao wataweza kupambana na CCM.

Mwisho kabisa kila aliyeshiriki kikao alipata Soda moja na fedha shilingi elfu tano.

Kuanzia hapo umejitokeza mgawanyiko mkubwa kati ya kundi la wanaomuunga mkono mch Msigwa kwa ushabiki, urafiki na posho ya shilingi elfu tano,na wale wanaodai kuwa hawawezi kuiacha CCM maana ndio mtetezi wao wanapokuwa na matatizo.
************MWISHO*************

Saturday, August 23, 2014

A LITTLE INSPIRATIONAL STORY TO SHARE..............!!!!!!!!!

A Magic Lesson To Success


There was some time ago, in a city, there lived a couple who have a comfortable
life. Both of them are living happily married. They have a secure job, own a
house, car and those common needs you can imagine.

Basically, this couple does not need to worry much about their financial or
relationship needs. But after living the same life style for years, they realized that
their life seems to be so routine! It is so predictable that it seems like something is
missing for both of them.

Everyday, they wake up in the morning, go to work, come back from work, go
home, eat dinner (sometimes they have to dine outside) watch tv, wash car and go
back to sleep. The normal, typical daily stuff. With the money they earned
everyday, it would not be possible for them to go on vacation overseas a lot, go
safaris in Africa or take flying lessons. You know, the lifestyle of the richer group
for whom spending money is not a main concern.

What is missing!!? Their passion in life….

This is because they have not sought the passion in their life and with their current
financial situation, this is the type of enjoyment they can afford to spend on.
So one day, the wife voiced out that she has had enough; enough is enough of this
meaningless life, they need to find their passion in life, to enjoy life to the fullest
and be better off financially. They know they can achieve more, but do not know
why they are not achieving more. Achieving does not mean that they have to be
millionaires, but in every other aspects of life. The husband agreed, and so they set
off to find a better lifestyle and seek the passion for their life.

And amazingly, the husband is told by a successful friend of his, that there is a
magical success guru living in a far, far away land, on top of the highest mountain
where there is a cave. The guru lives in that cave.
The husband is excited with this news, and so after much discussion with his wife,
they make a decision. They decide to seek advice from the guru for the secrets of
success. They take their company leaves, save some money for traveling and off
they go.

After months of searching high and low with their determination to seek the
answer, finally they find the mountain where the guru lives.
Excited as they are, they make their climbs to the peak of the mountain. It is very
hard and tedious, but it is worth the effort. Finally, they are at the peak.
Overseeing the view of the world from the top of the mountain, they feel so
confident and a peace of mind. Now, their task is to find the guru. The hard part is:
Where could he be? They think.

Suddenly, they see an old man, sitting at the end of the mountain rock. It seems
very dangerous to sit there, because anyone can fall off anytime down the
mountain and break all the bones. Of course, anyone who falls off will probably
end up dead with broken bones.

So, the wife whispers to the guru, 'Excuse me, old man, are you the magical
success guru that helps people to be successful?'
The guru seems not to be hearing her whisper. He is still sitting quietly at the end
of the mountain rock without any movement.

The wife whispers again. Then, the old man turns around and stands up at the end
of the mountain rock. This is even more dangerous now, because anyone can lose
balance and fall off!

Be careful, o'wise guru! You can fall down from the mountain rock if you stand
so near at the end of the edge!' they warn.
But the guru simply ignores what they say. In fact, he replies, 'If you want to speak
with me and learn from me, you have to come closer. Come and stand beside me
at the end of the mountain rock, my students-to-be.'

If they want to learn the secrets of success from the guru, they have to follow his
instruction. With a lot of fear, they come close to the guru. Now, the Guru is
standing in the middle with both of them standing on the left and right side of the
Guru. All 3 of them are facing outwards of the mountain, they are facing the down
slope of the mountain over looking the top of the world . They can fall down the
mountain at any time if they are not careful. The husband's and wife's hearts are
panting non-stop.

At this moment they feel so different, a feeling they never felt before, peace of
mind and yet full of anxiety. Looking down the land, they feel really confident.
And also a little bit afraid of falling off. It will break their bones if they fall down
the mountain.

The husband is thinking, 'Now what?'.
So, he asks the guru the million-dollar question,
'What is the secret of success, o'wise guru?'

The guru just smiles at them and replies, 'Look at the world beyond below, from
here.'

Following the instruction, both of them did as instructed, looking at the world
from the top of the mountain. They can see almost everything from the peak of the
mountain.

Suddenly, the guru pushes them off the mountain peak!! Unbelievable!
(Sad conclusion??)

Both of them fall.

When they fall, with so much fear of death, suddenly, they realize that they can
fly! And they fly…… because they have forgotten that they can fly all this
while...........

-------------------------------------------The End----------------------------------------------

Please take some time to digest the meaning of the story above,
and think what lessons are hidden behind the story
.

Some people can 'fly' but they had forgotten how to 'fly'.
So they forgot.

Some people completely do not know they can 'fly'.
So they never did

Some people had 'flown' before, but forgot how to.
So they never remembered.

Some people know they can fly, but never try because they
are surrounded by F-E-A-R.
So they quit.

Some people want to see others 'fly' first before they 'fly'.
So they waited.

Some people wait for a mentor to teach them how to fly.
So they waited.

Some people 'flew' before and fell down, so they claimed
that 'flying' is dangerous and useless. So they whined and quitted.

But, some people are 'flying' everyday, looking from below the
sky, overseeing everyone who is not 'flying' just because they
took a step to fly……

I had taken my 'flying' lessons and fell many times.

But now, I have discovered my wings again.

Have you started 'flying' yet?

Tuesday, August 19, 2014

CCM INAZIDI KUIMARIKA KILA MWAKA; KAULI ZA WAPINZANI NI SAWA NA DUA LA KUKU

UPINZANI KUONGOZA NCHI HII MIAKA HII NI SAWA NA MBOWE KUONYESHA CHETI CHAKE CHA FORM SIX KWA WAANDISHI WA HABARI.

Ni kwa wenye akili kubwa ambao akili zao ni zaidi ya GB 1000 ndio wanaoweza kukubaliana na mimi tu, hawa ambao akili zao zinasoma kwenye MB bado tuwaache kwenye vijiwe vya bangi na viroba wakisubiri Slaa (UKAWA) aingie IKULU.

Nasema hivi kwani takwimu zinanipa authority ya kufanya hivyo. Nimekuwa nikifuatilia siasa za nchi yangu toka enzi za kuchagua mtu na kivuli mimi sikuletwa kwenye siasa nay ale mafuriko ya Mrema 1995 wala haya ya padre Slaa na chopa mwaka 2010. Amini usiamini kuitoa CCM madarakani inahitaji zaidi ya karne mbili zijazo ila kwa namna ya upinzani tulio nao sahau kabisa.

Kama na wewe ni muumini kwa QUNTITATIVE ANALYSIS utakubalina na hiki ninachokisema hebu tuangalie data zinatuambia nini tangu kuanzishwa kwa mfumo wa vyama vingi hapa Tanzania 1992. Baada ya kuanzishwa mfumo wa vyama vingi nchini taifa kwa mara ya kwanza lilikwenda kwenye uchaguzi 1995 uchaguzi ambao ulishirikisha vyama vingi vya siasa. Upinzani ulionekana mkubwa kwa watu wawili MKAPA na MREMA japokuwa vyama vingine pia vilikuwepo. Katika uchaguzi uliofanyika Oktoba 29, 1995 Mgombea wa CCM Benjamin Mkapa alipata kura 4,026,422 wakati mgombea wa NCCR-Mageuzi Bw. Augustine Lyatonga Mrema alipata kura 1,808,616. Wapiga kura walikuwa ni 6,846,681. HIvyo, Mkapa alipata asilimia 61.82 wakati Mrema akipata asilimia 27.77

Baada ya uchaguzi huo Raisi mkapa aliingia madarakani na kuitoa Tanzania kutoka sehemu moja kwenda nyingine, kwa kifupi ni kwamba mkapa alifanya mambo makubwa sana katika kipindi chake cha kwanza jambo lililowapa wananchi imani kubwa sana juu yake na kumrudisha kipindi cha pili kwa ushindi mkubwa zaidi ukilinganishwa na ule wa mwaka 1995. Hakuna haja ya kuorodhesha mambo aliyoyafanya mkapa hapa kwani kila mtu anayajua.Uchaguzi wa Mwaka 2000 CCM ilifanya vizuri zaidi kuliko miaka mitano nyuma. Rais Mkapa alipata asilimia 71.74 ya kura zote za Urais 5,863,201 wakati Prof. Ibrahim Lipumba wa CUF akipata asilimia 16.26 ya kura za Urais 1,329,077 wakati Augustine Mrema akigombea mara ya pili akipata kura 637,077. Wapiga kura waliojiandikisha wakiwa 10,088,484 na waliopiga kura wakiwa 8,517,598 sawa na asilimia 84.4.Katika chaguzi zote hizi mbili CHADEMA hakikuwahi hata kushika number tatu wakati number moja imekuwa ikishikwa na ccm huku number mbili na tatu vyama vya CUF na NCCR vikibadilishana nafasi.

Mwaka 2005 CCM ikiwa imebadilisha mgombea kama katiba ya chama chake inavyosema iliendelea kungara huku vyama vingine vingi vikiendela kusimamisha wagombea wale wale waliendelea kuwa wapambe wa bwana harus CCM Kana ilivyo kawaida mpambe kazi yake ni kumsindikiza bwana harusi kila mahali ila ikifika muda wa kulala huwa nje ya kuta nne za chmba cha bwana harusi ndivyo hivyo kwa wapinzani walikuwa wakiishia kwenye sherehe za kuapishwa pale uwanja wa uhuru. Katika uchaguzi huu wa mwaka 2005 bendera ya ccm ikipeperushwa na Jakaya Mrisho Kikwete mgombea wa ccm alipata kura 9,123,952 sawa na asilimia 80.28 wakati mgombea wa upinzani Prof. Lipumba akipata kura 1,327,125 wakati Freeman Mbowe akipata kura 668, 756 sawa na asilimia 5.88.Kwa mara ya kwanza CHADEMA ikijitokeza kwenye 3 bora huku wakiambulia kura 668, 756 sawa na asilimia 5.88 sawa na idadi ya wakazi wa wilaya moja kwa baadhi ya wilaya za Tanzania.

Mwaka 2010 Rais Kikwete alipata kura 5,276,827 sawa na asilimia 62.83 wakati Dr. Slaa mgombea wa CHADEMA akipata kura 2,271,941 sawa na asilimia 27.05 ya kura za Rais huku Prof. Lipumba akipata asilimia 8.28 ya kura za Rais. Kutoka kura 9,123,952 alizopata mwaka 2005 hadi kura 5,276,827 ni anguko kubwa kwani alipoteza angalau kura milioni 3,847,125. Katika uchaguzi huu ile mamluki ya NCCR ikawa imehamia chadema na kukifanya kushika nafasi ya pili. Hapa kwa mwana CCM yoyote atakubaliana na mimi kuwa asilimia za ushindi kwa vipindi vyote ilishuka zaidi ila kuna sababu zake mojawapo ya sababu hizo ni:-

1. Baada ya kipindi cha kwanza cha uongozi wa JK wananchi walikuwa wanatarajia kasi zaidi ya maendeleo kuizidi ile ya Mkapa ila hawakujua kuwa JK ni muumini safi wa strategic plan yaan mipango ya muda mrefu. Utakubaliana na mimi kuwa baada ya kushinda mwaka 2005 JK alikuwa anajikita zaidi kutengeneza mipango ya muda mrefu ya kimaendeleo na ambayo ni sustainable. Utakubalina na mimi kuwa mipango hiyo ndio inayowezesha kukamilika kwa utekelezaji wa ilani ya CCM ya mwaka 2010 kwa asilimia zaidi ya 85. Kutokana na kipindi hiki kuwa ni cha kutengeneza mipango kilishusha moral ya wananchi kwa CCM kidogo.

2. Sababu ya pili ya asilimia hizi kushuka ni ukweli usiopingika kwamba pamoja na kwamba muasisi wa sera ya UKWELI NA UWAZI ni MKAPA ila mtekelezaji wake mkuu alikuwa KIKWETE. Ndani ya miaka mitano ya JK mambo mengi maovu yaliwekwa wazi wananchi wakajua mfano UFISADI si kwamba huko nyuma lilikuwa halipo lilikuwepo toka enzi za Nyerere ila kulikuwa hakuna fursa za kujua mambo hayo, kuingia kwa JK madarakani na kuvipa vyombo vya habari uhuru zaidi ndio chanzo cha haya mambo kujulikana. Kutokana na hali hiyo na kutokana na wananchi kuamini kuwa viongozi wao ni wema kimaadili wakati wote walipokuja kugundua kuwa baadhi yao ni wanyonyaji walikichukia chama na kutaka kulipiza kisasi kwa kumchagua slaa wakiamini kuwa ni padre na hawezi kuwanyonya. Ikumbukwe kuwa JK alilifanya hili kwa nia njema tu ya kutaka kuleta uwajibikaji (accountability).
Nadiriki kusema kuwa si kwa kuwa upinzani ni bora zaidi ndio ulioleta tofauti hii ya mwaka 2005 na 2010 bali ni RISK alizozibeba JK katika kuileta CCM mpya na tunayoitaka.

Kuelekea mwaka 2015 dalili zote za awali zimeshaonyesha kuwa CCM ndiye mshindi wa uchaguzi huo hata wakinisimamisha mimi hapa nitashinda. Hili limeonwa hata na wanachadema wenyewe na hata mtunga ilani yao ya mwaka 2010 Dr KITILA ameliona. Katika andiko lake alilolipa jina la “CCM is stabilising, CHADEMA is shrinking and CUF is disappearing!” andiko la tarehe 11th February 2014, mwanazuoni huyu amejaribu kuonyesha jinsi chama chake kinavyokufa taratibu huku watawala wa ndani ya chama wakijaribu kuwaficha wanachama ukweli. Bila kuficha anachokiamini Dr Kitila alikuwa akiwataka wanachama pamoja na vongozi wa CDM kutumia matokeo ya chaguzi ndogo wa kuanzia mwaka 2010 hadi 2014 kujipima na kujitathimini QUNTITAVELY kama chama kina gain au kina lose. Msomi huyu akitumia uchaguzi wa madiwani wa kata 27 wa mwezi wa pili 2014 amechambua matokeo yale quantitavely na kuonyesha ni kwa namna gani CDM inasinyaa kila kukicha huku CCM ikiimarika kwa kasi ya ajabu. Mfano kwa kutumia uchaguzi huo kati ya kata 27 CCM ilishinda kata 23 huku chadema ikiambulia kata 3 na NCCR kata 1. Ukijumlisha idadi ya wapiga kura wote kwa kata zote CCM ilipata idadi ya kura asilimia 85, CDM asilimia 11 na NCCR asilimia 1. Matokeo haya yapo karibu mno na uchaguzi mkuu ujao 2015.
Dr kitila hakuishia hapo kuwathibitishia watanzania kuwa chadema inasinyaa msinyao wa karatasi ya nailoni iliyokutana na moto wa gesi alitumia matokeo ya mwaka 2012 ya kata 29 zlizogombewa katika uchaguzi huo uliofanyika November 2012 CCM ilishinda kata 22 CDM kara 5 huku kata mbili zikienda vyama vingine. Msomi huyu alitumia data hizi na kuzilinganisha na hizi za 2014 ndipo alipogundua kuwa CCM inaimarika kila kukicha wakati CDM ikisinyaa.

Hapa tukitumia tena matokeo ya ubunge kwenye majimbo mawili ya KALENGA na CHALINZE utaona kuwa kusoma kunamzidi mpiga ramli kwani Kitila anazidi kudhihirisha alichokisema tarehe 11/2/2014.
Kuelekea mwaka 2015 CCM imezidi kuimarika zaidi pale ilipobadilisha safu yake ya uongozi. Safu hii ikiwa na mtendaji mkuu katibu Kinana, naibu wake bara Mwigulu na mwenezi wa chama Nape imekuwa ni mwiba mchungu sana kwa upinzani. Wameshtukia hili wanakuja kwa sura ya UKAWA.

Tumeshawasoma mapema nina wasiwasi hata idadi ya wabunge wenu itapungua mwaka 2015.